|
Taasisi ya Saratani ya jijini Ocean Road imeanza kuzidiwa
2009-01-24 12:04:06
Na ITV Habari
Taasisi ya Saratani ya jijini Ocean Road imeanza kuzidiwa kutoa huduma za tiba hiyo kwa wagonjwa wapya kutokana na idadi ya wagonjwa hao kuongezeka kila mwaka na kufikia wagonjwa elfu arobaini wanaohitaji tiba hiyo kwa mwaka .
Wakizumgumza baada ya ufunguzi wa mkutano wa siku tatu kujadili mikakati ya kuthibiti ugonjwa wa saratani uliohudhuriwa na wataalam wa tiba na madkatari wa saratani nchini baadhi ya washiriki wamesema kuna haja ya kuongeza jitihada katika kuwahamasisha wanajamii wa maeneo ya vijijini umuhimu wa kuwahi tiba ya saratani ikiwa kwenye awamu za mwanzoni wakati bado kuna matumaini ya mgonjwa huyo kupona.
|