|
Kuna haja ya kila mfanyabiashara kujiunga katika vikundi na vyama vinavyohusika na maeneo ya biashara
2009-04-17 14:37:30
Na IT Habari
Baraza la taifa la biashara nchini TNBC limesema kuna haja kwa kila mfanyabiashara kujiunga katika vikundi na vyama vinavyohusika na maeneo ya biashara ili kuleta chachu ya ukusanyaji kodi katika kuisaidia serikali kukusanya mapato ambayo kwa sasa yamekuwa yakipotea.
Wito huo umetolewa jijini Dar es Salaam na katibu mtendaji wa baraza hilo Bw dunstan Mrutu wakati na mazungumzo yake na wajumbe wa kamati ya bunge ya viwanda ,biashara na masoko.
|